NYARAKA ZA ELIMU

HOME USAJILI DARASA VII-2012=NECTA MATOKEO YA MTIHANI WAKUMALIZA ELIMU YA MSINGI TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI 2010/2011 MATOKEO YA MITIHANI MUHULA WA PILI-2011 KUMBUKUMBU ZA UONGOZI SAFU YA UONGOZI MASWALI YA JIOGRAFIA VIONGOZI WA SERIKALI YA WANAFUNZI KALENDA YA SHULE RATIBA YA SHULE IDADI YA WANAFUNZI MALI ZA SHULE PICHA ZA SHULE WANAFUNZI WASIO NA SARE MAWASILIANO PICHA ZA SHULE MTIHANI WA ENGISH-STD III MTIHANI FORM TWO NYARAKA ZA ELIMU Photo Blog MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK - KATA YA ILOLANGULU.MARCH-2013



1

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413, 2120403/4/

5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb.Na. TTDB/85/483/01/25

S.L.P. 9121

DAR ES SALAAM

Tarehe: 02/12/2009

Katibu Mkuu,

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali,

ZANZIBAR.

Katibu Mtendaji,

Baraza la Mitihani la Tanzania,

S.L.P. 2624,

DAR ES SALAAM.

KUH: MIHTASARI YA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI NA

STASHAHADA ILIYOREKEBISHWA NA UTARATIBU WA KUTAHINI

Rejea barua yenye Kumb. Na. TIE/MIN/ED/180/CA/IX/55 ya tarehe 3/9/2009

kuhusu shauri lililotajwa hapo juu.

Napenda kukuarifu kuwa tumepokea mihtasari ya aina nne (mipya na

iliyoboreshwa). Mihtasari iliyoboreshwa ni:

„X Mihtasari ya Ualimu ngazi ya Stashahada

„X Mihtasari ya Ualimu ngazi ya Cheti

Mihtasari miwili mipya ni:

„X Mihtasari ya Elimu kwa Michezo (Cheti)

„X Mihtasari ya Elimu ya Awali (Cheti)

Malengo ya jumla ya Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada ni

kuandaa walimu wenye sifa walio na ujuzi na maarifa katika kufundisha Elimu ya

Msingi na ya Sekondari.

Mihtasari ya mafunzo ya ualimu ngazi ya Stashahada ilikuwa inatekelezwa kwa

miaka 2: mwaka mmoja wa mafunzo chuoni na mwaka mmoja wa mazoezi ya

kufundisha shuleni. Aidha, mihtasari mipya ngazi ya cheti (kawaida) inafuta

2

matumizi ya mihtasari ya awali iliyokuwa inajumuisha masomo ya Maarifa ya

Jamii. Mihtasari ya Elimu kwa Michezo na ile ya Elimu ya Awali ni mipya.

Mihtasari yote minne ipo tayari kwa kutumika sasa kwa utaratibu wa mafunzo ya

miaka miwili chuoni. Mategemeo ni kwamba kupitia mafunzo ya ualimu wahitimu

watapata maarifa, ujuzi na stadi ili kumudu vema kazi ya kufundisha.

Utaratibu wa kutahini mihtasari ya stashahada ulikwisha tolewa kupitia barua

Kumb. Na. TTDB/193/437/OIA/6 ya tarehe 05/05/2008. Pamoja na ufafanuzi

kupitia barua Kumbukukumbu Na. TTDB/109/374/01/26 ya tarehe 6/7/2009.

Maelekezo ya kutahini yameweka mkazo katika: malengo, ujuzi maarifa stadi

muhimu, masomo ya kutahini, sifa zinazostahili kwa watahiniwa na viwango vya

utambuzi (‘distinction’, ‘credit’, ‘pass’ and ‘fail’). Kwa hiyo utahini wa mihtasari ya

ualimu ngazi ya cheti uzingatie misingi hii pia.

Sifa na muda wa mafunzo

Sifa ya chini ya kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi za Cheti (Cheti cha Ualimu,

Elimu ya Awali, Elimu kwa Michezo) bado itabaki ufaulu wa “Division IV” alama

28. Sifa za ziada za kujiunga na mafunzo ya ualimu Elimu ya Awali na

Elimu kwa Michezo zitaandaliwa na zitatolewa rasmi na kuanza kutumika mwezi

Julai, 2010.

Sifa kwa wale wanaojiunga na mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada kuanzia

tarehe 1 Julai 2009 ni “Principal pass” moja na “Subsidiary” moja katika masomo

yanayofundishwa shule za sekondari. Utaratibu huu ulikuwepo na utaendelea

mpaka itakapoelekezwa vinginevyo.

Sifa kwa wanaojiunga na mafunzo ya Stashahada ya Ualimu fani ya ufundi

itaendelea kuwa cheti cha FTC. Hata hivyo kwa lengo la kutoa fursa kwa

wahitimu wenye ufaulu mzuri katika masomo ya Sayansi na Hisabati, wasio na

cheti cha FTC wanaweza kujiunga na Stashahada ya Ualimu ya kawaida. Aidha,

kufuatia ‘phasing out’ ya programu ya FTC wenye sifa ya ‘NTA level 6’ na ambao

wangependa kusomea ualimu wanaweza kujiunga na ‘Diploma in Technical

Education’ wakati wale wa ‘NTAlevel 5’ watajiunga na Stashahada ya kawaida.

Utaratibu huu utatuwezesha kupata walimu wa fani hii na pia kutopoteza

wahitimu wenye ufaulu mzuri katika masomo ya Sayansi na Hisabati kwa ajili ya

shule za sekondari zenye mchepuo wa ufundi.

Muda wa mafunzo ya ualimu kwa programu zote (cheti cha ualimu, Elimu ya

Awali, Elimu kwa Michezo na Stashahada) utakuwa miaka 2.

3

Utambuzi na masharti ya kurudia

Kama ilivyopendekezwa awali, kwa mitihani ya ngazi zote za ualimu, ufaulu wa

kila mtahiniwa upimwe katika viwango vya madaraja manne (‘Distinction’,

‘Credit’, ‘Pass’ and ‘Fail’).

Katika ngazi ya Stashahada mtahiniwa atakayeshindwa masomo yasiyozidi nusu

ya masomo yote aliyotahiniwa katika mtihani ataruhusiwa kurudia. Mtahiniwa

atakayeshindwa masomo mawili ya kufundisha hataruhusiwa kurudia na atakuwa

ameshindwa. Vilevile mtahiniwa atakayeshindwa Mazoezi ya Kufundisha

hataruhusiwa kufanya mtihani na atakuwa ameshindwa. Mtahiniwa ataruhusiwa

kurudia masomo aliyoshindwa katika muda usiozidi miaka miwili tangu afanye

mtihani wa awali na fursa hii ni mara moja tu. Aidha anayerudia mitihani

anatakiwa afaulu masomo yote aliyorudia.

Mitihani ya mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti, Elimu kwa Michezo na Elimu ya

awali haitakuwa na utaratibu wa kurudia mitihani kwa wanachuo

watakaoshindwa mitihani mara ya kwanza.

Utahini wa Mafunzo ya Sayansi, TEHAMA na Lugha

Utaratibu wa kupima maendeleo ya kila siku ya mwanachuo uimarishwe, uwe na

uzito unaostahili na uwe wazi zaidi.
Mafunzo kwa Vitendo (Practicals) kwa

masomo ya Sayansi, TEHAMA na Lugha (English) yataimarishwa na

mwongozo utatolewa mara baada ya maandalizi kukamilika.

Pamoja na maelezo haya, utaratibu wa kutahini ulioandaliwa na kuanza kutumika

katika mihtasari ya stashahada ya mwaka 2009 uzingatiwe.

Kwa mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti mabadiliko haya yana lengo la kuandaa

mwalimu anayemudu kufundisha masomo yote ya shule za msingi. Wanachuo

waandaliwe kufundisha masomo yote wakiwa mwaka wa kwanza. Watakuwa na

fursa ya kuchagua somo la ziada (option) wakiwa mwaka wa pili. Masomo ya

uchaguzi (options) yatatahiniwa pamoja na masomo ya lazima. Masomo ya

kuchagua ni pamoja na Vielelezo na Teknolojia, Commnication Skills, ICT na

Lugha za kigeni (mfano Kifaransa).

Pamoja na maelezo haya naambatanisha maelekezo kuhusu idadi ya mitihani

kwa kila ngazi ya mafunzo (Kiambatisho A). Aidha, orodha ya masomo ngazi ya

Stashahada, Cheti ngazi ya shule za Msingi, Elimu ya Awali na Elimu kwa

Michezo imeambatanishwa (Kiambatisho B).

4

Maelekezo haya yanaanza kutumika kuanzia tarehe 1 Julai 2009 na yatawahusu

wanachuo walioanza mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti na stashahada mwezi

Julai 2009. Aidha, yatakuwa msingi wa kutahini kuanzia mitihani ya Mei 2011.

Nakutakia utekelezaji mzuri.

Umesainiwa na:

A. S. Mrutu

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala

1. Mkurugenzi, Taasisi ya Elimu Tanzania.

S. L. P. 35094

DAR ES SALAAM

2. Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

TANZANIA BARA

3. Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

TANZANIA BARA

5

KIAMBATISHO A

Aina ya mafunzo ya Ualimu na mitihani yake, ujuzi stadi na maarifa ya kuzingatia katika kutahini.

Aina ya

mafunzo ya

Ualimu

Ujuzi, maarifa na stadi za kuzingatia Idadi ya mitihani na maeneo ya

kutahini

1. Elimu ya

Msingi

„X Ujuzi, unaoshirikisha wanafunzi kujifunza

„X Kuongoza wanafunzi wenye mahitaji tofauti

katika kujifunza

„X Kuandaa na uwezo wa kutumia zana za

kufundishia na kujifunza kwa usahihi

„X Uwezo na maarifa katika kushughulika na

masuala mtambuka

„X Kujali na kuwasaidia wanafunzi wa shule za

msingi

„X Kuonyesha umahiri wa kufundisha masomo

yafundishwayo shule msingi

„X Matumizi ya vielelezo na TEHAMA

„X Somo la Ualimu (mtihani 1)

Masomo ya Taaluma

„X Masomo ya lazima: Geography,

Historia, Uraia, Kiswahili, English,

TEHAMA, Haiba na Michezo,

Hisabati, Sayansi, na Stadi za Kazi.

* Masomo ya kuchagua

(chagua somo moja):

-
Vielelezo na Teknolojia,

Communication Skills, ICT, French

2. Elimu kwa

Michezo

„X Ujuzi unaoshirikisha wanafunzi kujifunza

michezo

„X Kuongoza wanafunzi wenye mahitaji tofauti

katika kujifunza ngazi ya msingi

„X Kuandaa na kutumia zana za kufundishia na

kujifunza michezo

„X Uwezo na maarifa katika kushughulika na

maswala mtambuka

„X Kujali na kuwasaidia wanafunzi wa shule za

msingi kukuza vipaji katika michezo

„X Kuonyesha umahiri wa kufundisha michezo

shule za msingi

„X Matumizi ya vielelezo na TEHAMA

„X Ualimu Michezo (mtihani 1 –

lazima)

„X Masomo mawili ya Elimu kwa

Michezo:

- Michezo (mtihani 1 lazima)

- Usimamizi na Usalama katika Michezo

(mtihani 1 – lazima)

„X Masomo ya lazima (Taaluma na

Ufundishaji – mtihani 1)

- Uraia

- Communication Skills

- Sayansi

6

- TEHAMA

- English

- Kiswahili

- Hisabati

* Masomo ya kuchagua: Chagua

somo moja kati ya: French au lugha

nyingine, ICT, Vielelezo na Teknolojia.

3. Elimu ya

Awali

„X Ujuzi wa kutumia njia zinazoshirikisha

wanafunzi kujifunza

„X Kujadili na kuwasaidia wanafunzi wa elimu ya

Awali

Mitihani ya mwisho itakuwa na jumla ya

mitihani 10

(a) Somo la Ualimu (mtihani 1)

(b) Masomo ya Taaluma (lazima)

„X Communication skills (mtihani 1)

„X Uraia (mtihani 1)

* Chagua somo moja kati ya:

„X Vielelezo na Teknolojia;

„X ICT

( C) Vitendo vya kufundishia na

kujifunzia (vitendo 6)

„X Vitendo vya Hisabati (Taaluma +

Ufundishaji)

„X Vitendo vya sanaa (Taaluma +

Ufundishaji

„X Vitendo vya Kiswahili (Taaluma +

Ufundishaji)

„X Vitendo vya Haiba na Michezo

(Taaluma + Ufundishaji)

„X Vitendo vya Sayansi (Taaluma +

Ufundishaji)

„X English Learning activities

(Academic + Pedagogy)

7

KIAMBATISHO B

Orodha ya Mihtasari ya Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada

1. Education Psychology Guidance and Counselling

2. Currículum and Teaching

3. Foundation of Education

4. Education Research, Measurements and Evaluation

5. Education Media and Technology

6. Communication Skills

7. French Academic Syllabus

8. French Pedagogy syllabus

9. English Academic Syllabus

10. English Pedagogy syllabus

11. Muhtasari wa Utaalamu wa Kufundislha somo la Kiswahili

12. Muhtasari wa Taaluma wa somo la Kiswahili

13. Information and Communication Technology Syllabus

14. Information and Computer Studies

15. Physics Academic Syllabus

16. Chemistry Academic Syllabus

17. Chemistry Pedagogy Syllabus

18. Chemistry Pedagogy syllabus

19. Biology Academic Syllabus

20. Biology Pedagogy Syllabus

21. Mathematics Academic Syllabus

22. Mathematics Pedagogy Syllabus

23. Geography Academic Syllabus

24. Geography Pedagogy Syllabus

25. History Academic Syllabus

26. History Pedagogy Syllabus

27. Development Studies Syllabus

28. Civics Pedagogy Syllabus

Orodha ya Mihtasari ya Ualimu ngazi ya Cheti kwa Elimu ya Msingi, Michezo na Awali

A. Elimu ya Msingi

1. Ualimu Elimu ya msingi

2. Vielelezo na Teknolojia

3. Communication Skills

4. English

5. Kiswahili

6. French

7. Stadi za Kazi

8. Jiografia

9. Uraia

10. Historia

11. Sayansi

12. Hisabati

13. ICT

14. TEHAMA

15. Haiba na Michezo

8

B. Elimu kwa Michezo

1. Ualimu Michezo

2. Michezo

3. Usimamizi na Usalama katika Michezo

C. Elimu ya Awali

1. Ualimu Elimu ya Awali

2. Vitendo vya Masomo ya Elimu ya Awali

9

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb.Na. ED/OKE/NYK/2010/2

S.L.P. 9121

DAR ES SALAAM

Tarehe: 22 Februari, 2010

Makatibu Tawala wa Mikoa,

Makatibu Tawala Wilaya,

Wakurungenzi; Halmashauri za Miji/Manispaa/Jiji,

Wakurugenzi Watendaji; Halmashauri za Wilaya,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya,

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi,

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 2 WA MWAKA 2010

VITABU VYA KIADA SHULENI

Mwaka 1991 Wizara ya Elimu na Utamaduni ilitoa sera kuhusu upatikanaji na

usambazaji wa vitabu shuleni na vyuoni. Sera hii ambayo ilianza kutumika tarehe

1 Januari 1992 inahalalisha mfumo wa matumizi ya kitabu zaidi ya kimoja cha

kiada katika shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu ili mradi vitabu hivyo

viwe vimepata ithibati. Utaratibu huu hauweki ukomo au madaraja ya ubora wa

vitabu vilivopata ithibati. Hali hii imesababisha kuwepo kwa vitabu vingi vya kiada

vilivyopata ithibati kushindania soko.

Wizara imebaini kuwa kutokana na hali hii shule zinajikuta zikitumia vitabu vya

kiada tofauti. Aidha, kwa kuwa uwezo wetu wa kununua vitabu shuleni ni mdogo,

imebidi shule nyingi zichague kitabu kimoja au viwili kama vitabu vya kiada bila

kuwa na fursa ya kuona vitabu vyote vilivyopewa ithibati katika masomo husika ili

ziweze kufanya uchaguzi muafaka. Kwa maana hiyo, wanafunzi walikosa fursa

sawa ya kupata maarifa kutoka katika chaguo pana la vitabu vilivyopewa ithibati

na hatimaye kusababisha kukosekana kwa ulinganifu wa ubora wa ufundishaji na

ujifunzaji.

10

Kufuatia hali hii, Wizara inapitia upya utaratibu huo wa matumizi ya kitabu zaidi

ya kimoja cha kiada kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kuwa mabadiliko hayo

hayataleta athari katika utoaji wa elimu nchini.

Wakati utaratibu huo unapitiwa, Wizara imeamua kwamba kila Somo na kila

Darasa husika litakuwa na vitabu viwili teule vya kiada ili kuhakikisha kwamba

vitabu vya kutosha vinapatikana shuleni. Vitabu vya kiada vilivyochaguliwa kwa

sasa ni vile vya ngazi ya Elimu ya Awali na ngazi ya Elimu ya Msingi kwa Darasa

la Kwanza hadi laTano.

Orodha ya vitabu hivyo imeambatishwa na Waraka huu. Vitabu vya Darasa la

Sita na la Saba havitahusika kwa sasa, hivyo utaratibu uliokuwepo utaendelea

kutumika. Aidha, vitabu vyote vyenye ithibati ambavyo havikuchaguliwa kutumika

kama vya kiada vitatumika kama vitabu vya rejea na ziada katika kujifuna na

kufundishia.

Utaratibu wa kuteua vitabu vya kiada kwa Darasa la Sita na la Saba na kwa

ngazi ya Sekondari na Vyuo vya Ualimu unaandaliwa.

Wizara inaomba ushirikiano kutoka kwa wadau wote katika kutekeleza

mabadiliko hayo.

Waraka huu unaanza kutumika mara moja.

Umesainiwa na:

A. S. Mrutu

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

11

Kiambatisho A.

VITABU VILIVYOPENDEKEZWA

12

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR

ES SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL. 1/01

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 28/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Maafisa Elimu wa Msingi wa Wilaya

TANZANIA BARA

WARAKA WA ELIMU NA. 1 WA MWAKA 2011

MASOMO YATAKAYOTAHINIWA KATIKA MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU

YA MSINGI

Masomo yanayofundishwa katika Elimu ya Msingi ni Hisabati, Kiswahili, English,

Sayansi, Historia, Jiografia, Stadi za Kazi, TEHAMA, Uraia, Haiba na Michezo,

Kifaransa na Dini. Kati ya masomo hayo, masomo ya lazima ni Hisabati,

Kiswahili, English, Sayansi, Historia, Jiografia, Dini, Uraia, Stadi za Kazi, Haiba

na Michezo.

Aidha, masomo ya Kifaransa TEHAMA na Dini ni ya ziada (optional). Kutokana

na umri na uwezo wa kujifunza wa mwanafunzi wa shule ya msingi, masomo

haya ni mengi kwake kuyamudu na kuyafanyia mtihani.

Kwa msingi huo, Wizara iliamua kuwa masomo yatakayotahiniwa katika mtihani

wa kuhitimu Elimu ya Msingi ni Hisabati, Kiswahili, English, Sayansi na Maarifa

(Historia, Jiografia na Uraia) na yatatahiniwa kwa muda wa siku mbili mfululizo.

Msimamo wa Wizara ni kuendelea kutahini masomo hayo. Masomo mengine

yatafundishwa kikamilifu bila kutahiniwa.

Waraka huu unaanza kutumika mara moja

13

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

14

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR

ES SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb.Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/02

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 29/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Maafisa Elimu Msingi/Sekondari wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA

WARAKA WA ELIMU NA. 2 WA MWAKA 2011

TARATIBU ZA UANDIKISHAJI WANAFUNZI/WANACHUO KWA KUZINGATIA

URAIA

Imebainika kuwa kuna baadhi ya wanafunzi wanaoandikishwa katika shule za

serikali na zisizo za serikali bila kubainishwa uraia wao na hivyo kusababisha

watu hao kusoma na kuajiriwa kama raia wa Tanzania baada ya kuhitimu

masomo/kozi zao. Hali hii imesababishwa na uandikishaji wa wanafunzi

usiozingatia kipengele cha uraia wao.

Kutokana na hali hiyo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inaagiza

kuzingatiwa kwa taratibu za uandikishaji wa wanafunzi katika ngazi zote za elimu

kwa kuzingatia kipengele cha uraia wa wanafunzi. Kwa hiyo kila mwanafunzi

anayeandikishwa ni
lazima aoneshe cheti cha kuzaliwa au uthibitisho wa uraia

wake.

Utaratibu huu utasaidia kutambua uraia wa wanafunzi na wanachuo.

Waraka huu unaanza kutumika Januari, mwaka 2012.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

15

Nakala:

1. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

2. Wizara ya Mambo ya Ndani

3. Wakurungenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

4. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

16

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na ED/OKE/NYE/VOL.1/03

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 29/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Maafisa Elimu wa Msingi/Sekondari wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA

WARAKA WA ELIMU NA. 3 WA MWAKA 2011

KUZOROTA KWA UTAMADUNI WA KUJISOMEA VITABU KWA WALIMU NA

WANAFUNZI

Kusoma vitabu na makala mbalimbali ni mojawapo ya njia ya kupata maarifa kwa

mtu yeyote. Kujisomea vitabu ni njia muhimu sana kwa walimu na wanafunzi ili

kukuza stadi ya kufundishia na kujifunzia.

Utamaduni huu wa kujisomea vitabu na makala mbalimbali miongoni mwa

walimu na wanafunzi umekuwa ukizorota siku hadi siku. Hali hii, imesababisha

baadhi ya walimu kushindwa kufundisha ipasavyo na wanafunzi kuwa tegemezi

kwa maarifa yanayotolewa na walimu wao. Ikumbukwe kwamba ili wanafunzi

waweze kujifunza vizuri, wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika mchakato mzima

wa kujifunza ikiwa ni pamoja na kuibua na kutetea hoja zao.

Madhumuni ya waraka huu, ni kusisitiza kufufua utamaduni wa kujisomea vitabu

na makala mbalimbali kwa walimu na wanafunzi ili kuboresha mawanda ya

ufundishaji na ujifunzaji.

Kwa kuzingatia mazingira ya shule husika, kila mkuu wa shule/mwalimu mkuu

ahakikishe wanafunzi na walimu wanajenga tabia ya kujisomea vitabu na makala

mbalimbali.

17

Kwa waraka huu inaagizwa kuwa, maktaba za shule zifufuliwe na pale ambapo

hazikuwepo zianzishwe.

Waraka huu unaanza kutumika Januari, 2012

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

18

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/04

S. L. P. 9121

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 28/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Maafisa Elimu wa Msingi/Sekondari wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu,

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 4. WA MWAKA 2011

KUDHIBITI JANGA LA MOTO KATIKA SHULE NA VYUO VYA UALIMU

NCHINI

Siku za hivi karibuni janga la moto limekuwa likijitokeza mara kwa mara katika

shule. Janga hili limesababisha maafa na hasara kubwa kwa serikali na jamii

ikiwemo kupoteza mali na maisha ya wanafunzi.

Wizara imechunguza sababu za kuwepo kwa janga la moto na kubaini kuwa

baadhi ya shule huendeshwa bila kuzingatia mambo muhimu ya kudhibiti janga

hili la moto. Kujihami na janga hili ni suala linalohitaji kuweka mikakati thabiti ya

kupambana na janga hili. Katika kudhibiti janga hili la moto, Wizara ya Elimu na

Mafunzo ya Ufundi, inawahimiza wadau wa elimu hususan walimu wakuu wa

shule za Msingi, Wakuu wa shule za Sekondari na Vyuo vya Ualimu kuhakikisha

kuwa asasi zote za elimu zinatekeleza mambo yafuatayo:

„h Kuwa na vifaa vya kuzimia moto na vihisi moshi (smoke detectors)

vinavyofanya kazi na vinakaguliwa mara kwa mara;

„h Kuwa na mifumo ya nyaya za umeme iliyo madhubuti na inayokaguliwa

mara kwa mara;

„h Kuwepo kwa milango ya dharura inayofunguka kwa nje katika majengo

yote yanayokusanya watu pamoja mfano, mabweni, maabara na bwalo la

chakula/mikutano;

19

„h Kila asasi ipige marufuku matumizi ya vibatari na mishumaa ndani ya

mabweni/daharia;

„h Kuhakikisha kuwa hakuna msongomano wa wanafunzi katika

mabweni/daharia;

„h Kuwapatia wanafunzi elimu ya tahadhari ya milipuko ya moto na majanga

mengine; na

„h Kuhakikisha kuwa wanafunzi hawapiki wala kupiga pasi ndani ya

mabweni/daharia kwa kutumia pasi za mkaa na umeme, kitengwe chumba

maalum kwa ajili ya kupigia pasi.

Maafisa Elimu wa Halmashauri wanashauriwa kufuatilia utekelezaji wa suala hili

katika Halmalshauri zao.

Waraka huu unaanza kutumika Januari, 2012

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

20

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na.ED/OKE/NYE/VOL.1/05

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 28/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Maafisa Elimu wa Msingi/Sekondari wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu,

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 5 WA MWAKA 2011

UTARATIBU WA KUWASIMAMISHA/KUWAFUKUZA SHULE WANAFUNZI

WATORO KATIKA SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO VYA UALIMU

Pamekuwepo na ukiukwaji wa kanuni na taratibu za kushughulikia kesi za

wanafunzi watoro shuleni/vyuoni. Baadhi ya walimu wakuu na wakuu wa

shule/vyuo wamekuwa na utaratibu usiozingatia maelekezo kuhusu uendeshaji

wa shule/vyuo kama zilivyoanishwa kwenye kiongozi cha mwalimu mkuu na

mkuu wa shule/chuo kwa kujichukulia hatua mkononi kwa kuwasimamisha na

kuwafukuza wanafunzi hao. Hali hii imesababisha kuwepo kwa malalamiko

miongoni mwa wanajamii, na kama itaachwa iendelee itasababisha usumbufu

mkubwa kwa pande zinazohusika.

Kutokana na hali hiyo, wizara imelazimika kutoa waraka kukemea tabia hii.

Kuanzia sasa ni marufuku kwa mwalimu mkuu au mkuu wa shule/chuo

kumsimamisha/kumfukuza shule mwanafunzi mtoro bila kuzingatia taratibu

zilizowekwa. Kama mwanafunzi hatafika shuleni/chuoni kwa muda wa siku 30

mfululizo bila kutoa taarifa kwa uongozi wa shule/chuo atasimamishwa masomo,

na kama ataendelea kuwa mtoro hadi kutimia
siku 90 mfululizo atafukuzwa

shule na kikao halali cha kamati / bodi ya shule/chuo.

21

Kwa upande wa makosa mengine ya kinidhamu kanuni na taratibu zilizoanishwa

kwenye kiongozi cha mwalimu mkuu na mkuu wa shule/chuo zitaendelea

kutumika.

Waraka huu unaanza kutumika mara moja.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

22

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/06

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 27/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Wakuu wa Shule za Sekondari/Vyuo

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 6 WA MWAKA 2011

KUPIGA MARUFUKU UTITIRI WA MITIHANI

Mtihani ni njia inayotumiwa kumwezesha mwalimu kujua kiwango cha uelewa wa

wanafunzi kuhusu mada zilizofundishwa kwa kipindi fulani.

Kumezuka mtindo wa baadhi ya walimu kutunga mitihani mbalimbali na

kuwapatia wanafunzi bila kuzingatia madhumuni ya mitihani katika mchakato

mzima wa kujifunza. Walimu hao wanatunga mitihani na kuwapa wanafunzi

wafanye kwa kulipia fedha kitendo hicho ni kinyume na taratibu na maadili ya

ufundishaji.

Aidha, mitihani hii hufanyika kila mara kitendo kinachopunguza muda mwingi wa

ufundishaji, mitihani hiyo ni kama: `speed test’, Mitihani ya Wiki, Mitihani ya

Ujirani Mwema na Mitihani ya Mwezi. Mitihani yote hii wanafunzi huchanga

fedha.

Ili kupunguza utitiri wa mitihani, Wizara inashauri mitihani ifuatayo ndio itiliwe

mkazo.

„h Mitihani ya Nusu Muhula

„h Mitihani ya Muhula

„h Mitihani ya Mwezi

Aidha, mitihani hii ifanyike bila kuchangisha fedha wanafunzi.

23

Kwa Waraka huu ninaagiza kuacha mara moja kuwapa wanafunzi mitihani

inayotolewa bila lengo maalumu. Mazoezi ya darasani yatumike kupima uelewa

wa mada zilizofundishwa.

Mwalimu yeyote atakayebainika akichangisha fedha kwa kisingizio cha

kugharimia mitihani atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.

Waraka huu unaanza kutumika mara moja.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

24

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/07

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 29/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Awali/Msingi

TANZANIA BARA

WARAKA WA ELIMU NA. 7 WA MWAKA 2011

UBORESHAJI WA ELIMU YA MAZINGIRA YA SHULE/VYUO

Mazingira ni vitu vyote vinavyoizunguka jamii.

Mazingira mazuri shuleni huleta uelewa wa haraka kwa mwanafunzi na motisha

kwa mwalimu katika ujifunzaji na ufundishaji kwa kutumia mifano halisi iliyo

katika mazingira ya shule. Hivyo, mazingira mazuri ni kivutio kwa shule na jamii.

Ili kuhifadhi mazingira na kuleta mandhari nzuri ya shule vitu kama usafi,

michezo mbalimbali, bendi ya shule na gwaride vinaongeza mvuto.

Wizara inawakumbusha Maafisa Elimu wote, Wakuu wa Shule za Msingi,

Sekondari na Vyuo vya Ualimu kuhimiza utekezaji wa yafuatayo:-

„h Kupanda miti (miti ya kivuli, matunda, mbao na kuni)

„h Kupanda maua

„h Kupanda ukoka/nyasi

„h Kupanda ‘hedges’ pembeni mwa barabara zote za shule

„h Kupanda mawe na kuyapaka chokaa

„h Kuweka mipaka thabiti ya shule

„h Kuboresha na kuanzisha miradi mbalimbali

„h Kutengeneza viwanja, kufufua na kudumisha michezo mbalimbali

„h Kufufua na kudumisha bendi za shule

„h Kutayarisha ramani za: -

25

(a) Wilaya yao katika eneo la shule kwa kutumia vifaa vinavyopatikana

kwa urahisi katika mazingira yao

(b) Mkoa wao

(c) Tanzania

(d) Afrika

(e) Dunia

„h Kuingiza dhana za Elimu ya Mazingira katika masomo yote

yanayofundishwa shuleni.

„h Kuingiza dhana za Elimu kwa Maendeleo Endelevu katika masomo yote

yanayofundishwa shuleni.

„h Kutumia vyombo/vifaa vya kisayansi kufanya utafiti katika mazingira.

„h Kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, Siku ya Kunawa Mikono Duniani,

n. k.

„h Kutupa taka zikiwa zimechambuliwa katika sehemu maalum (taka

zinazooza, taka zisizooza, plastiki, maji machafu, chupa, n. k.)

„h Kuhakikisha kuwa chakula kinatunzwa katika sehemu safi na zisizoruhusu

wadudu na sumu kufikia chakula hicho.

Waraka huu unarekebisha Waraka Na. 11 wa mwaka 1998 na unaanza

kutumika mara moja.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais

3. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

26

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/08

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe : 29/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa,

Makatibu Tawala wa Wilaya,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya,

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu,

Wakuu wa Shule za Sekondari,

Walimu Wakuu wa Shule za Awali/Msingi,

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 8 WA MWAKA 2011

KUKITHIRI KWA MICHANGO SHULENI

Wizara ilitoa Waraka wa Elimu Namba 2 wa Mwaka 1999 wenye Kumb. Na.

ED/OK/C.2/4/50 uliohusu michango ya kuendeleza shule.

Tangu kipindi hicho hadi sasa imebainika kwamba, baadhi ya shule zisizo za

serikali na hata za serikali zimekuwa zikiendelea kutoza wazazi michango

kiholela hata pale isipostahili na bila kibali cha wizara au Kamati za shule, Bodi

za shule na Halmashauri husika. Michango hii imekuwa ni kero kubwa kwa

wazazi na wanafunzi na hata kusababisha baadhi ya wanafunzi kuacha shule na

wengine kuwa watoro.

Aidha, baadhi ya michango inayodaiwa ni ya kununulia vifaa vya kujifunzia na

kufundishia kujenga majengo na samani. Baadhi ya shule hutoza michango ya

majengo kila mwaka, ingawa majengo hayo hayaendelei kujengwa au vifaa na

samani hizo haziongezeki badala yake upungufu wa vitu hivyo huendelea

kuwepo shuleni. Pia kutoza michango mbalimbali ya mitihani isiyo na idadi.

Uwingi wa michango isiyoratibiwa ni kinyume cha taratibu na inaongeza mzigo

kwa wazazi na kusababisha wanafunzi kukosa masomo pale wanapofukuzwa

kwa kutolipa michango hiyo.

27

Kwa Waraka huu, Wizara inaagizwa kuwa Michango yote ya maendeleo ya shule

idhibitiwe kwanza na
Wanajamii wote, Kamati ya Shule/Chuo, Bodi yaShule/Chuo na Halmashauri husika. Aidha, utaratibu wa kukusanya michango

hiyo usihusishe wanafunzi.

Shule yoyote ambayo itahitaji kuchangisha wazazi michango, ni sharti wazo hilo

lijadiliwe na Kamati/Bodi ya shule na wazazi washirikishwe kwenye kikao cha

walimu ili maoni yatolewe.

Maombi ya kuchangisha michango ni budi yatumwe kwenye Halmashauri husika

ambapo kibali kitatolewa au kukataliwa. Michango yote iliyokubaliwa

kuchangishwa itatolewa na wanajamii au wazazi na sio wanafunzi. Jukumu la

kukusanya michango litabaki mikononi mwa wanajamii, hivyo jamii iandae

taratibu zao za kuhakikisha michango waliyopitisha wenyewe inachangishwa bila

kuwabughudhi wanafunzi.

Aidha, kwa shule zisizo za serikali zisitoze wanafunzi michango ya aina yoyote

ya maendeleo ya shule kwani shule binafsi ni rasilimali ya mwenye shule.

Michango ambayo ni kero ni kama ifuatavyo:

„h Michango ya kuandikisha wanafunzi Darasa la Kwanza/Kidato cha

Kwanza.

„h Barua za utambulisho wa wanafunzi wanaofaulu Darasa la Saba kwenda

shule za sekondari.

„h Barua zote za wanafunzi kuitwa kujiunga na shule za sekondari / vyuo.

„h Fomu za kujiunga na Kidato cha Kwanza katika shule zisizo za serikali.

Inaagizwa kuwa barua zote za kuitwa kujiunga na shule zipitiwe na kupata kibali

cha Mkaguzi Mkuu wa Shule wa Wilaya/ Kanda husika baada ya kuridhika kuwa

michango inayoagizwa imepata kibali cha Halmashauri husika.

Waraka huu unafuta nyaraka zote za nyuma zinazohusu michango ya

kuendeleza shule na unaanza kutumika mara moja.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

28

Nakala:

1. Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani Tanzania

2. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI

3. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

29

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413, 2120403/4/

5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/10

S.L.P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 29/04/2011

Makatibu Tawala Mikoa,

Makatibu Tawala Wilaya,

Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania,

Wakaguzi Wakuu wa Shule (K),

Maafisaelimu wa Mikoa,

Maafisaelimu wa Wilaya, Msingi na Sekondari,

Wakaguzi Wakuu wa Shule (W),

Wakuu wa Shule za Sekondari zisizo za Serikali,

Walimu Wakuu wa shule za Msingi zisizo za Serikali,

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 10 WA MWAKA 2011

MASHARTI MAPYA YA USAJILI WA SHULE

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ndiyo msimamizi wa Elimu nchini kwa

mujibu wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 na sheria ya Elimu Na.25

ya Mwaka 1978 na rekebisho lake Na. 10 la Mwaka 1995.

Kuanzia mwanzoni mwa mwaka 1980 serikali iliruhusu wadau mbalimbali

wakiwemo watu binafsi na Taasisi zisizo za Serikali kutoa elimu katika ngazi

mbalimbali za elimu hapa nchini zikiwemo:- Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na

Vyuo vya Mafunzo ya Ualimu

Serikali inapongeza juhudi za wadau mbalimbali mathalan mashirika ya dini,

taasisi mbalimbali, watu binafsi na Halmashauri kwa kuitika wito huo.

Hata hivyo, mashirika, taasisi mbalimbali na watu binafsi wenye uwezo wa

kuanzisha shule zisizo za serikali hapa nchini, wanashauriwa kuzingatia masharti

yaliyoainishwa katika sheria na miongozo mbalimbali inayotolewa na Wizara.

Mwenye nia na uwezo wa kuanzisha Shule/Chuo cha ualimu ni lazima atimize

masharti yafuatayo:-

30

„h Awe na eneo lisilopungua Hekta 3 kwa maeneo ya vijijini na 1.5 kwa eneo

la mjini lililotolewa kwa madhumuni ya Elimu na Mamlaka husika (Wizara

ya Ardhi na Serikali za vijiji).

„h Aombe kibali cha kujenga majengo ya shule/chuo kwa kufuata ramani

zilizopendekezwa na Wizara ama zitakazokubaliwa na Wizara na ambazo

zimepitishwa na mamlaka za Halmashauri husika (Mhandisi wa Wilaya na

Mipango Miji wa Wilaya).

„h Akamilishe majengo muhimu ya mwanzo yakiwemo madarasa ya

kutosheleza wanafunzi wa mwaka wa I na II, jengo la utawala/ofisi za

walimu, bwalo/ukumbi, maabara moja kwa kuanzia, maktaba, vyoo vya

wasichana, wavulana na wafanyakazi na samani.

„h Aombe kuthibitishwa kuwa Mwenye Shule/chuo na Meneja wa Shule kwa

kujaza fomu Na. RS 6 na RS 7 na kuziwasilisha kwa Afisa Elimu wa

Wilaya/Mji/Manispaa ilipojengwa shule kwa maoni na mapendekezo. Pia

Mwenye Shule/chuo mtarajiwa atatakiwa kuwaomba Maafisa wa Afya,

Mhandisi wa Majengo na Mkaguzi Mkuu wa Shule (wote wa Wilaya)

Mji/Manispaa wafanye ukaguzi na taarifa zao zitatumiwa kuona hali halisi

na utayari wa majengo na mazingira ya shule/chuo.

Baada ya Mwenye Shule/Chuo na Meneja kuthibitishwa atajaza fomu na. RS. 8

ya kuomba kusajili Shule/Chuo. Fomu hii itawasilishwa kwa Mkaguzi Mkuu wa

Shule wa Kanda shule ilipojengwa.
Endapo shule ina sifa stahili itasajiliwa na

kupewa namba ya usajili na ndipo itaruhusiwa kuandikisha wanafunzi.

Tendo la kusajili litakuwa endelevu, na litajirudia kila baada ya miaka minne (4) ili

kuhakikisha kwamba viwango vilivyowekwa vinazingatiwa.

Shule/Chuo kitasajiliwa iwapo kitakuwa kimetimiza masharti yote ya usajili na

kupewa namba ya mtihani.

Waraka huu unafuta nyaraka zote za nyuma na unaanza kutumika kuanzia

Januari, 2012.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote , Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

31

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/11

S.L.P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe 29/04/2011

Makatibu Tawala Mikoa,

Makatibu Tawala Wilaya,

Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Wilaya/Miji/Manispaa/Jiji

Wakaguzi Wakuu wa Shule (K),

Wakaguzi Wakuu wa Shule (W),

Wakuu wa Shule za Sekondari,

Walimu wakuu shule za Msingi,

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 11 WA MWAKA 2011

UENDESHAJI WA MITIHANI YA KUMALIZA NGAZI MBALIMBALI ZA ELIMU

KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU

Wanafunzi wenye mahitaji maalumu wamekuwa wakijumuishwa kwa muda wote

wa kujifunza darasani. Kwa mujibu wa Waraka huu, wanafunzi wenye ulemavu

wanaolengwa ni wale ambao ulemavu wao umethibitishwa na mamlaka kuanzia

shule hadi wizara kuwa wanahitaji huduma inayokusudiwa.

Yamekuwepo malalamiko toka kwa wazazi wa wanafunzi wenye ulemavu kuwa

waendesha mitihani hawazingatii mahitaji ya kundi hili la watahiniwa.

Ili kuwawezesha kufanya mitihani kama wanafunzi wenzao maandalizi ya

mitihani, ufanyaji wake na usahihishaji lazima utambue mahitaji maalumu

waliyonayo wanafunzi wenye ulemavu.

Mahitaji hayo yapo katika maeneo yafuatayo:

„h Wasioona hutumia muda mwingi kuchomoa na kupachika karatasi kwenye

mashine ya kuandikia.

„h Wenye ulemavu wa viungo hupata shida ya kuandika (kitetemeshi) au

waendapo kujisaidia hutumia muda mrefu kurudi katika chumba cha mtihani

na wengine kuandika kutumia miguu au kichwa.

32

„h Wenye ulemavu wa akili kufikiri polepole hadi kupata kitu cha kuandika.

Waanzapo kuandika kasi yao ya kuandika ni ndogo.

„h Wenye uoni hafifu (wakiwemo Albino) husoma kwa shida maandishi ya

kawaida, hivyo kuhitaji maandishi yaliyokuzwa.

„h Viziwi hupata shida ya kutafsiri lugha ya kawaida kwa kuitenganisha na

lugha yao ambayo kwa kawaida sarufi huwa na makosa. Matatizo hayo

yanasababisha mahitaji ya muda zaidi. Hivyo waraka huu unawapa

nyongeza ya muda wa dakika 20 kwa kila saa ya somo la Hisabati na

dakika 15 kwa kila saa ya masomo mengine ya mtihani.

Kutokana na utaratibu huu wenye ulemavu waandaliwe mkondo wao, wenye

wanafunzi pekee ili ratiba iweze kufuatwa kwa urahisi.

Aidha, kuhusu usimamizi, inaagizwa wanafunzi wenye ulemavu wasimamiwe

na mwalimu mtaalamu wa Elimu maalum kulingana na aina ya ulemavu

uliopo shuleni.

Wakati wa kusahihisha mitihani hii, walimu watalamu wa wanafunzi wenye

ulemavu wahusishwe ili kushauri katika kazi hiyo kuwezesha utekelezaji wa

masuala hayo, maelekezo yote toka Baraza la Mitihani la Tanzania yazingatie

maelekezo hayo ili kuwezesha utekelezaji fanisi wa waraka huu.

Waraka huu unaanza kutumika Mara moja

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

33

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/12

SANDUKU LA POSTA

9121

DAR ES SALAAM

Tarehe 29/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Awali/Msingi

TANZANIA BARA

WARAKA WA ELIMU NA. 12 WA MWAKA 2011

KUKARIRISHA DARASA KUHAMISHA AU KUFUKUZA WANAFUNZI WA

SHULE ZA SEKONDARI

Imebainika kwamba, kuna shule za sekondari hasa zisizo za serikali,ambazo

zinaendelea kukaririsha darasa, kuhamisha au kuwafukuza shule wanafunzi bila

kufuata utaratibu uliotolewa, hata baada ya kutolewa Waraka namba 2 wa

mwaka 1997 na Waraka namba 6 wa mwaka 2007.

Ninapenda kuwakumbusha kwamba, muundo wa elimu ya sekondari katika

Tanzania Bara ni miaka minne kwa elimu ya sekondari ya kawaida na miaka

miwili ya elimu ya sekondari ya juu. Mwanafunzi anapochaguliwa kusoma katika

shule ya sekondari, anatakiwa asome kwa mfululizo kuanzia kidato cha kwanza

hadi cha nne na kuanzia kidato cha tano hadi cha sita.

Hayo ndiyo matarajio ya serikali, wazazi/walezi na wanafunzi wenyewe.

Umezuka mtindo wa baadhi ya Wakuu wa Shule zisizokuwa za serikali

kuwakaririsha wanafunzi, kuwahamisha au kuwafukuza shule kwa kisingizio

kwamba hawakufikia wastani wa shule.

Wizara inawakumbusha kwamba, kufanya hivyo ni kinyume cha matarajio ya

serikali wazazi/walezi na wanafunzi, kwani kunawaongezea mzigo wazazi,

34

kuwapotezea muda wanafunzi na kulifanya taifa lishindwe kufikia malengo ya

milenia na malengo ya elimu kwa wote.

Kwa Waraka huu, ninaagiza kwamba kuanzia sasa hakuna shule

itakayoruhusiwa kukaririsha, kuhamisha au kufukuza mwanafunzi kwa sababu ya

kutokufikisha wastani uliowekwa na shule.

Ili kuhakikisha agizo hili linafanikiwa, kila shule itatakiwa kufanya yafuatayo

wakati wa kuandikisha wanafunzi wa Kidato cha Kwanza na cha Tano:

„h Kila tarehe 31 Machi ya kila mwaka, Mkuu wa shule atatakiwa awe

amewasilisha orodha ya wanafunzi wote aliowaandikisha Kidato cha

Kwanza katika shule yake Baraza la Mitihani Tanzania, Wizara ya

Elimu na Mafunzo ya Ufundi na OWM-TAMISEMI

„h Kila tarehe 30 Aprili ya kila mwaka, Mkuu wa shule atatakiwa awe

amewasilisha orodha ya wanafunzi wote aliowaandikisha Kidato cha

Tano katika shule yake Baraza la Mitihani Tanzania, Wizara ya Elimu

na Mafunzo ya Ufundi na OWM -TAMISEMI.

Orodha hizi zitakazowasilishwa zitatoa takwimu halisi za wanafunzi

walioandikishwa kwa mwaka husika na hata kama mwanafunzi atahamishwa

kwa sababu yoyote ile itajulikana ametoka shule gani na amekwenda shule gani.

Aidha, takwimu hizi zitalisaidia Baraza la Mitihani la Tanzania kuweza kupanga

mipango yake ya baadaye pamoja na kutambua shule zinazofanya vizuri kwa

kuweza kufaulisha wanafunzi kwa kulinganisha walioandikishwa na waliomaliza

(Completion Rate).

Taratibu nyingine za kukariri zitafuata maelekezo kama ifuatavyo:-

„h Mwanafunzi anayeomba na kukubaliwa kukariri katika ngazi yasekondari Kidato cha I - IV atapewa fursa ya kukariri mara moja.

Endapo mamlaka inayohusika itaona umuhimu wa mwanafunzi

kukariri darasa ataweza kupewa fursa ya
kukariri mara mbili.

Hakuna mwanafunzi atakayeruhusiwa kukariri darasa zaidi ya mara

mbili katika ngazi hii. Kwa wale wanaosoma katika Kidato cha V na

VI watapewa fursa ya kukariri mara moja tu. Wizara inasisitiza

kwamba maombi yatakayokubaliwa ni yale ambayo kutokana na

sababu mbalimbali mwanafunzi amekosa masomo
kwa siku 90 auzaidi mfululizo kwa kukosa ada au kuwa mgonjwa na ugonjwa

ukathibitishwa na daktari.

Uamuzi huu utatekelezwa kama ifuatavyo:

„h Waombaji wanaosoma Kidato cha I - II, III au V watatakiwa

kuandika barua za maombi ya kukariri darasa kwa Katibu Tawala

wa Mkoa kupitia kwa Mkuu wa Shule anakosoma.

35

„h Maombi, kwa wale wanaotaka kukariri kidato cha IV au VI

yapelekwe kwa Kamishna wa Elimu kupitia kwa Mkuu wa Shule

wanakosoma wanafunzi.

„h Kila barua ya maombi ni lazima iwe na viambatisho vifuatavyo:

„h Picha 2 “passport size”

„h Nakala ya fomu ya maendeleo ya mwanafunzi.

„h Uthibitisho wa sababu ya kukariri, kwa mfano: -

a) Nakala ya vyeti vya matibabu na barua ya daktari alikotibiwa

mwanafunzi

b) Fomu namba 3 ya polisi (PF3) au barua ya Mahakama kwa

maswala ya jinai

c) Nakala ya barua ya uhamisho wa mzazi/mlezi.

d) Nakala ya barua toka kwa mzazi/mlezi kuwa mwanafunzi

amekosa ada

Waraka huu unasisitiza utekelezaji wa
Waraka Na. 6 wa Mwaka 2007, na

utaanza kutumika tarehe 1 Januari mwaka 2012.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

„h Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani Tanzania

„h Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI

„h Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

„h Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kandana Wilaya.

36

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.1/14

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 28/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Maafisa Elimu wa Msingi/Sekondari wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Awali/Msingi

TANZANIA BARA

MWONGOZO WA UVAAJI WA SARE ZA SHULE NA MWONEKANO

NADHIFU WA WANAFUNZI/WANACHUO

Kumejitokeza ukiukwaji wa sheria na kanuni za uendeshaji wa shule/vyuo

hususan katika uvaaji wa sare za shule na usafi wa mwili. Baadhi ya wanafunzi

wamekuwa wakivaa sare zinazokiuka taratibu za shule, mfano, kuvaa nguo za

kubana na fupi kwa wasichana na milegezo kwa wavulana. Aidha, baadhi ya

wanafunzi wanafuga na kupaka rangi kucha, wanafuga ndevu, kuwa na nywele

ndefu pamoja na mapambo mbalimbali.

Kutokana na kukithiri kwa hali hiyo katika baadhi ya shule, Wizara imelazimika

kuwakumbusha walimu wakuu wa shule za msingi, wakuu wa shule za sekondari

na vyuo vya Ualimu kuzingatia na kusimamia sheria na kanuni za uendeshaji wa

shule/vyuo zilizopo ili kulinda maadili na nidhamu shuleni/vyuoni.

Kwa waraka huu, inaagizwa kuwa mwanafunzi anatakiwa kuvaa sare ya shule

ipasavyo, na awe nadhifu kwa kuwa na nywele fupi, kukata kucha, kutopaka

rangi kucha, na kunyoa ndevu. Aidha, wasichana wawe na nywele fupi au

kusuka nywele za mistari kwenda nyuma.

Mwongozo huu usomwe sambamba na mwongozo kuhusu uvaaji wa hijab na

sala ya Ijumaa uliotolewa tarehe 18/08/1999.

37

Mwongozo huu, unaanza kutumika mara moja

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

38

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na ED/OKE/NYE/VOL.1/15

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 28/04/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Maafisa Elimu Msingi/Sekondari wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA

MWONGOZO WA UJAZAJI WA ALAMA ZA MITIHANI YA WANAFUNZI

KATIKA SEL FORMS NA TSM 9

Sel forms kwa wanafunzi wa sekondari na TSM 9 kwa wanafunzi wa shule za

msingi ni muhimu sana kwa sababu zinaonesha taarifa za maendeleo ya

mwanafunzi kitaaluma na kitabia. Taarifa zinazojazwa katika fomu hizi

zinatokana na alama za majaribio na mitihani ya mwisho wa mihula.

Pamekuwepo na ukiukwaji wa taratibu za ujazaji wa alama katika
sel forms na

TSM 9 kwa kujaza alama za kughushi. Hali hii husababisha kukosekana kwa

uwiano kati ya alama za maendeleo ya baadhi ya wanafunzi na matokeo yao ya

mitihani ya kitaifa.

Wizara inaagiza kuwa wakuu wa shule, walimu wakuu na walimu wote nchini

kuhakikisha kuwa wanazingatia taratibu na miongozo ya upatikanaji wa alama za

maendeleo ya kila siku ya mwanafunzi na kuzijaza ipasavyo kwenye fomu

husika.

Mwongozo huu unawakumbusha walimu wote kuzingatia maelezo

yaliyotolewa na unaanza kutumika mara moja.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

39

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

40

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb.Na. ED/OKE/193/292/02/86

S.L.P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 06/05/2011

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA

YAH: USIMAMIZI WA SHUGHULI ZOTE ZA SHULE

Wizara inatambua kazi nzito mliyonayo ya kusimamia shughuli za shule nchini.

Hata hivyo, imeona ni vyema kukumbushana katika baadhi ya maeneo.

Kumekuwepo na tabia ya baadhi ya walimu wakuu wa shule kutokuwepo katika

maeneo yao ya kazi kwa muda mrefu kwa kisingizio cha kuhudhuria semina na

mafunzo elekezi na kuacha shule ikiendeshwa na walimu wasaidizi au walimu

wa kawaida. Hali hii inasababisha kutokuwepo na usimamizi madhubuti wa

shule, na baadhi ya walimu kupata mwanya wa kutoingia madarasani na

kutofundisha wanafunzi ipasavyo.

Kwa barua hii wakuu wa shule, walimu wakuu wanatakiwa

„h Kuwepo shuleni siku zote 194.

„h Kuangalia ufundishaji wa walimu wakuu na ujifunzaji wanafunzi ili kuepusha

manung’uniko ya wazazi/walezi.

„h Kuhakikisha kwamba walimu wote wanafundisha ipasavyo kutokana na

madaraka waliyopewa.

Kama kutakuwepo na mafunzo elekezi, semina au vikao, ni vema shughuli hizo

zikaendeshwa wakati wa likizo fupi na ndef
u au wakati wa mwisho wa wiki. Hii

itawezesha wakuu wa shule, walimu wakuu kufanya kazi ya usimamizi wa shule

ipasavyo kutokana na madaraka waliyopewa.

Kwa yeyote atakayekiuka na kutofuata maazigo ya barua hii atachuliwa hatua za

kinidhamu.

41

Nakutakia kazi njema.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

3. Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

4. Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

5. Wakurugenzi; Halmashauri za Miji/Manispaa/Jiji

6. Wakurugenzi Watendaji; Halmashauri za Wilaya

7. Maafisa Elimu wa Mikoa

8. Maafisa Elimu wa Wilaya (Msingi/Sekondari)

9. Katibu Mkuu wa TAHOSSA

10.Katibu Mkuu, TAMONGSCO

42

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb.Na. ED/OKE/C.5/03/78

S.L.P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 14/07/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi wakuu wa shule wa Wilaya

Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Miji Manispaa na Jiji

Wakuu wa Shule za Sekondari

TANZANIA BARA

YAH: KIBALI CHA KUFANYA MTIHANI WA DINI YA KIISLAM KWA

WANAFUNZI WA DARASA LA SABA

Wizara ilipokea maombi kutoka “Islamic Education Panel’ kutaka kuwepo kwa

mtihani wa Dini wa Kitaifa kwa wanafunzi wa darasa la Saba.

Kwa kutambua umuhimu wa Somo la Dini kwa wanafunzi wetu Wizara imetoa

kibali Mtihani wa Dini ya Kiislamu kwa wanafunzi wanaohitimu Darasa la Saba

uanze kufanyika mwaka 2011.

Kwa mwaka 2011 mtihani huo utafanyika siku ya Jumatano, tarehe 10/8/2011.

Aidha, kila mwaka tarehe muafaka itakayofanyika siku ya Jumatano kila mwezi

Agosti itateuliwa. Mtihani huo utaendeshwa kwa gharama za “Ilamic Education

Panel”.

M.M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

1. Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

2. Wakurugenzi wote, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

43

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. OKE/NYE/VOL.I/19

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 16/12/2011

Makatibu Tawala wa Mkoa,

Makatibu Tawala wa Wilaya,

Wakurugenzi; Halmashauri za Miji/Manispaa/Jiji,

Wakurugenzi Watendaji; Halmashauri za Wilaya,

Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya,

Wakuu wa Shule za Sekondari,

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi.

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA. 14 WA MWAKA 2011

WANAFUNZI WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA WANAOCHAGULIWA

KUINGIA KIDATO CHA KWANZA KATIKA SHULE ZA SEKONDARI

KUTOPOKELEWA.

Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 imeainisha malengo ya Elimu ya

Msingi. Mojawapo ya malengo haya ni kumwezesha mwanafunzi kujifunza stadi

za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu.

Katika miaka ya hivi karibuni kumeibuka tatizo la kuwepo kwa wanafunzi

wasiojua Kusoma na Kuandika katika baadhi ya shule za sekondari. Hali hii

imeibua hisia nyingi miongoni mwa wadau wa elimu ikiwa ni pamoja na

kulalamikia umuhimu wa kuwepo kwa Mtihani wa Darasa la Nne na Kidato cha

Pili. Mitihani hiyo ni ya muhimu sana kwa wanafunzi kwani itaweza kuwachuja na

kupata wanafunzi wazuri na kuweka misingi bora ya wanafunzi katika ujifunzaji.

Ili kurekebisha dosari hii, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inaagiza wakuu

wa shule za Sekondari kutowapokea wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika

44

kujiunga na Elimu ya Sekondari. Aidha, wanafunzi watakaochaguliwa kujiunga

na elimu ya sekondari kila mwaka wafanyiwe jaribio la kupima stadi za kusoma,

kuandika na kuhesabu katika ngazi ya shule ya sekondari kabla ya kuanza

masomo yao rasmi. Zoezi hili lifanywe na wakuu wa shule katika shule ya

sekondari mwanafunzi alipochaguliwa. Zoezi hili ni la muhimu na lifanywe kwa

umakini ili kupata wanafunzi wenye sifa stahiki kuendelea na masomo ya

sekondari. Jaribio hili lisiwe na gharama zozote toka kwa wazazi hasa michango

ya fedha.

Mwanafunzi atakayeshindwa jaribio hilo hataruhusiwa kuanza masomo ya Elimu

ya Sekondari na endapo itagundulika kuwepo na udanganyifu katika Mtihani wa

kuhitimu Darasa la Saba ambao amefanya mwanafunzi husika, hatua za

kinidhamu zitachukuliwa kwa waliohusika na udanganyifu huo.

Waraka huu unaanza kutumika tarehe 1 Januari,2012.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala: Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.

Mkurugenzi, Taasisi ya Elimu Tanzania.

Wakurugenzi, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

45

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Cable: ELIMU DAR ES SALAAM.

PHONE: 2123686

Telex: 242741 Elimu Tz.

Email: escc@intafrica.com

Webaite:www.moe.go.tz

Reply please quote:

Kumb. Na. EB/OK/C.2/4/49

S.L.P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 28/12/2011

Makatibu Tawala wa Mikoa,

Wakurugenzi; Halmashauri za Miji/Manispaa/Jiji,

Wakurugenzi Watendaji; Halmashauri za Wilaya,

Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya,

Mameneja na wenye Shule,

Wakuu wa Shule za Sekondari

TANZANIA BARA

WARAKA WA ELIMU NA. 16 WA MWAKA 2011

WASTANI WA UFAULU KATIKA MTIHANI WA TAIFA KIDATO CHA PILI

Mtihani wa taifa Kidato cha Pili ulianzishwa mwaka 1984 kwa madhumuni ya

kupima maendeleo ya wanafunzi baada ya miaka miwili ya Elimu ya Sekondari.

Mtihani huu ni tathmini ya kati inayopima kiwango cha maarifa na ujuzi aliopata

mwanafunzi kutokana na masomo aliyojifunza katika Kidato cha Kwanza na cha

Pili. Aidha, unalenga kuwapatia motisha walimu na wanafunzi ili waongeze bidii

na kuinua viwango vya maendeleo ya wanafunzi kitaaluma.

Shabaha ya serikali ni kutoa elimu katika ngazi zote ikiwemo ya sekondari kwa

kuwafanya walimu na wanafunzi wawajibike ipasavyo. Mtihani wa Kidato cha Pili

ni njia mojawapo ya kuhakikisha kuwa wazazi, walimu na wanafunzi

wanawajibika ipasavyo.

Utafiti uliofanyika mwaka 2011 ulibainisha sababu mojawapo ya wanafunzi

kufanya vibaya ni kutokana na kuwaruhusu kuendelea na masomo hata baada

ya kushindwa kufikia alama ya ufaulu katika mtihani wa Kidato cha Pili. Aidha,

wanafunzi, wazazi, walimu na wadau wengine walionesha haja ya ufaulu wa

mtihani wa Kidato cha Pili kuwa kipimo cha kuendelea na masomo ya Kidato cha

Tatu.

46

Baadhi ya shule za sekondari zisizokuwa za serikali zimekuwa na alama tofauti

za ufaulu wa mtihani huo na kuwanyima fursa baadhi ya wanafunzi ya kuendelea

na masomo ya Kidato cha Tatu katika shule zao kwa alama za ufaulu

walizojiwekea.

Kwa mantiki hiyo, Wizara inaendelea kusisitiza kuwa kiwango cha alama ya

ufaulu ni 30%. Kiwango hiki ni kwa shule za serikali na zisizo za serikali.

Mwanafunzi ambaye atashindwa kupata alama hizo atalazimika kukariri kidato

cha pili mara moja tu na iwapo atashindwa kufikia alama ya ufaulu ataondolewa

katika mfumo rasmi wa elimu.

Waraka huu unarekebisha Waraka Na. 5 wa Mwaka 2008 na unaanza kutumika

Januari, 2012.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

„h Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI

„h Mkurugenzi, Taasisi ya Elimu Tanzania,

„h Wakurugenzi, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

47

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NE/VOL.1/01/8

S.L.P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 10/01/2012

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda,

Maafisaelimu Mikoa,

Maafisaelimu Wilaya (Sekondari),

Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali,

YAH:
MWONGOZO WA UTEKELEZAJI WA WARAKA WA ELIMU NA. 14 WA

MWAKA 2011 WA NAMNA YA KUTAHINI STADI ZA KUSOMA NA

KUANDIKA KWA WANAFUNZI WANAOJIUNGA NA KIDATO CHA

KWANZA

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inatoa mwongozo huu ili kuwa na

ulinganifu mzuri wa kutahini stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu kwa

wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari kuanzia mwaka 2012 kwa nchi

nzima. Wanafunzi wa chaguo la kwanza wapimwe mwezi Februari, na wale wa

chaguo la pili wapimwe mwezi Aprili kila mwaka.

Ili zoezi hili lifanyike kwa ufanisi itabidi mwanafunzi atahiniwe kwa utaratibu

akianza na kusoma, kuandika na hatua ya mwisho kuhesabu kwa kufanya

mojawapo ya yafuatayo:

Stadi Mazoezi Aendelee

Kusoma Kusoma kifungu (para) ya

hadithi kwa sauti (maneno 25)

Kusoma maneno

yasiyopungua 20 kama

inavyotakiwa

Kuandika imla (maneno 25) Aandike maneno

yasiyopungua 20 kama

inavyotakiwa

Kuandika

Kuandika hadithi fupi au barua

fupi

Aandike maneno vizuri

yanayosomeka na

kuleta maana

Kusoma na

Kuandika

Kusoma kifungu (para) cha

hadithi isiyo na misamiati

migumu na kujibu maswali 5

yaliyo wazi

Ajibu maswali 3

yanayohusu hadithi

hiyo kwa usahihi

48

Kuhesabu Hesabu 10 rahisi za

kujumlisha, kutoa, kuzidisha na

kugawa

Afanye hesabu 8 kwa

usahihi

Kuhesabu na

kuandika

Apewe picha za maumbo 5

(duara, mstatili, pembetatu,

mstari, miraba)

Aandike majina ya

maumbo hayo kama

inavyotakiwa

Mkuu wa shule akishirikiana na walimu atayarishe mazoezi hayo kwa lugha ya

Kiswahili na Kingereza ili mwanafunzi atahiniwe kwa lugha aliyotumia katika

elimu ya msingi.

Aidha, zoezi hili lihusishe walimu wote katika shule ili líweze kukamilika ndani ya

siku moja. Majina ya watahiniwa watakaoshindwa yawasilishwe kwa Afisaelimu

Mkoa.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

49

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Kumb. Na.
CHA-281/478/01/56 Tarehe: 01/02/2012

Makatibu Tawala wa Mkoa,

Makatibu Tawala wa Wilaya,

Wakurugenzi; Halmashauri za Miji/Manispaa/Jiji,

Wakurugenzi Watendaji; Halmashauri za Wilaya,

Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya,

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu,

Wakuu wa Shule za Sekondari,

TANZANIA BARA

WARAKA WA ELIMU NA. 1 WA MWAKA 2012

KUREJESHWA KWA ADA YA MTIHANI KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA

SERIKALI

Uendeshaji wa Mitihani ya Taifa una shughuli mbalimbali zinazohitaji fedha

nyingi. Kwa miaka yote, Serikali huchukua sehemu kubwa ya gharama za

kuendesha mitihani ya kitaifa ikiwa ni pamoja na gharama za utunzi, uchapaji,

usambazaji, usimamizi, usahihishaji na uchambuzi wa matokeo. Sehemu

nyingine ya gharama hizi inachangiwa na watahiniwa wenyewe.

Mwaka 2009, Serikali ilisitisha uchangiaji katika mitihani ya Kitaifa kwa wanafunzi

wote wa shule za Serikali wanaofanya mitihani ya Kidato cha 2, Kidato cha 4 na

Kidato cha 6. Watahiniwa wa kujitegemea (Private Candidates) na wa shule

binafsi ambao ni asilimia ndogo ya watahiniwa ndio walioendelea kuchangia

gharama za mitihani.

50

Kwa kuwa gharama za uendeshaji wa mitihani zimeendelea kuwa kubwa mwaka

hadi mwaka, Serikali imeamua kurudisha ada za Mitihani kwa shule za Serikali ili

kuchangia gharama. Watahiniwa watalipa Ada za mitihani kama ifuatavyo:-

Mtihani wa Kidato cha 2 sh. 10,000/= kila Mtahiniwa

Mtihani wa Kidato cha 4 sh. 35,000/= kila Mtahiniwa

Mtihani wa Kidato cha 6 sh. 35,000/= kila Mtahiniwa

Ada hizi zitalipwa na wanafunzi wote wa shule za Serikali, shule zisizo za serikali

na watahiniwa wa kujitegemea. Ada hizi zitaanza kulipwa kwa mitihani yote ya

kitaifa (Kidato cha 2, 4, 6) itakayoanza mwaka 2012/13.

Baraza la Mitihani litatoa maelekezo zaidi kuhusu tarehe za kufanya malipo

hayo.

Kwa kuwa michango ya watahiniwa ni sehemu tu ya gharama stahili, Serikali

itaendelea kuchukua sehemu kubwa ya gharama za uendeshaji wa mitihani ya

Kitaifa.

Waraka huu unaanza kutumika mwaka wa fedha 2012/13 na unafuta waraka Na

1 wa mwaka 2010.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala : Katibu Mkuu Kiongozi,

Ofisi ya Rais, Ikulu

S. L. P. 9120

DAR ES SALAAM

Katibu Mkuu,

Ofisi ya Rais,

Idara Kuu ya Utumishi wa Umma,

S. L. P. 2483

DAR ES SALAAM

Katibu Mkuu,

OWM - TAMISEMI,

S. L. P. 1923,

DODOMA

51

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL. 1/15

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 06/02/2012

Makatibu Tawala wa Mkoa,

Makatibu Tawala wa Wilaya,

Wakurugenzi; Halmashauri za Miji/Manispaa/Jiji,

Wakurugenzi Watendaji; Halmashauri za Wilaya,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda,

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya,

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu,

Wakuu wa Shule za Sekondari,

Waratibu Elimu Kata,

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi.

WARAKA WA ELIMU NA. 2 WA MWAKA 2012

UMUHIMU WA WALIMU KUHUDHURIA VIPINDI DARASANI NA

KUFUNDISHA

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inatambua wajibu wa walimu katika

kutekeleza azma ya Serikali ya kulipatia Taifa huduma ya Elimu nchini. Aidha,

wizara inaheshimu jitihada na uvumilivu unaonyeshwa na walimu katika

kutekeleza azma hii ya serikali pamoja na kwamba mara nyingi elimu inatolewa

katika mazingira magumu. Wizara inawapongeza wale wote wanaotekeleza

wajibu wao kwa moyo wa kujituma na wa kizalendo.

Pamoja na jitihada zinazoonyeshwa na walimu wengi, wapo walimu wachache

ambao wana tabia ya kuondoka shuleni na kuacha wanafunzi bila msaada

wowote wa kujifunza kwa visingizio kuwa wanafuatilia shida zao katika ofisi za

elimu Mkoani au Wilayani/Halmashauri. Aidha, baadhi ya walimu huondoka

shuleni na kuwatelekeza wanafunzi kwa madai kwamba wanakwenda

kuhudhuria mikutano ambayo haina uhusiano au haichangii kuboresha utoaji wa

elimu.

52

Hali hii inalelewa na baadhi ya walimu wakuu, wakuu wa shule na wakuu wa

vyuo vya ualimu ambao wanaona utovu huu wa nidhamu ukiendelea bila

kuchukua hatua zinazostahili kukomesha tabia hiyo. Tabia nyingine ni ile ya

kuwaacha wanafunzi bila kufundishwa licha ya mwalimu kuwepo shuleni. Tabia

hii inakiuka maadili ya ualimu na kuvunja sheria na kanuni za utumishi.

Kutokana na hali hii, Wizara inaagiza kuwa mwalimu yeyote ambaye

hatafundisha vipindi vyake bila sababu za msingi atachukuliwa hatua za kisheria

ikiwa ni pamoja na kukatwa mshahara wake kwa kipindi chote ambacho

hakuhudhuria vipindi na kufundisha. Aidha, mwalimu mkuu, mkuu wa shule/chuo

cha ualimu ahakikishe kuwa walimu wanahudhuria vipindi na kufundisha

wanafunzi ipasavyo ili kuleta ufanisi.

Ripoti ya mwalimu atakayeshindwa kutimiza wajibu wake ipelekwe mara moja

kwa Mkurugenzi wa Wilaya/Halmashauri husika kwa ajili ya kuchukuliwa hatua

za kinidhamu.

Waraka huu unawakumbusha walimu kuwa ni watumishi wa serikali ambao

wameajiriwa chini ya sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa serikali na

utumishi wa walimu (TSD), hivyo wanapaswa kufuata na kuzingatia sheria na

kanuni hizo katika ufundishaji na ujifunzaji wa wanafunzi darasani.

Ni matumaini ya wizara kuwa walimu wakuu, wakuu wa shule/vyuo vya ualimu

watatoa ushirikiano unaostahili kwa walimu ili kuboresha elimu nchini.

Waraka huu unarekebisha Waraka wa Elimu Na. 14 wa mwaka 1997 na utaanza

kutumika mwaka 2012.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala: Katibu Mkuu OWM – TAMISEMI.

53

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

Anuani ya Simu: ELIMU DAR ES

SALAAM.

Simu: 2120402, 2120413,

2120403/4/ 5/7/8/9

Telex: 42741 Elimu Tz.

Fax: 2113271 Elimu Tz

Unapojibu tafadhali taja:

Kumb. Na. ED/OKE/NYE/VOL.I/18

S. L. P. 9121,

DAR ES SALAAM.

Tarehe: 21/05/2012

Makatibu Tawala wa Mikoa

Makatibu Tawala wa Wilaya

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Kanda

Wakaguzi Wakuu wa Shule wa Wilaya

Wakuu wa Vyuo vya Ualimu

Wakuu wa Shule za Sekondari

Walimu Wakuu wa Shule za Msingi

TANZANIA BARA.

WARAKA WA ELIMU NA 3 WA MWAKA 2012

WANAFUNZI KUFUKUZWA SHULE/CHUO KABLA YA MTIHANI WA TAIFA

KUFANYIKA

Sheria ya Elimu ya mwaka 1978 na Rekebisho lake Sura ya 353 Kifungu Na.

35(3) ya mwaka 2002, inaeleza kuwa kila mwanafunzi akijiandikisha shule hana

budi kuhudhuria na kumaliza shule katika ngazi husika. Aidha, mipango yote ya

Elimu: Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi [MMEM] na Mpango wa

Maendeleo ya Elimu ya Sekondari [MMES], inasisitiza wanafunzi kuandikishwa,

kuhudhuria na kumaliza masomo yao katika ngazi husika.

Pamoja na kwamba ni lazima wanafunzi walioandikishwa kuhudhuria na

kumaliza masomo katika ngazi husika ya elimu, baadhi ya shule/vyuo

wamekuwa na utamaduni wa kuwasimamisha au kuwafukuza shule/chuo

wanafunzi wakati mitihani inapokaribia kutokana na makosa mbalimbali ya utovu

wa nidhamu. Kamati au Bodi za Shule/Chuo hutoa adhabu ya kuwafukuza

wanafunzi hao shule/chuo wakati wanakaribia kufanya mitihani yao ya mwisho

kwa ajili ya kuhitimu ngazi husika ya masomo.

Matatizo mengi ya utovu wa nidhamu yangeweza kushughulikiwa mapema na

shule au chuo badala ya kusubiri wakati mitihani inapokaribia. Kitendo cha

54

kufukuza wanafunzi wakati mitihani inapokaribia kinasababisha usumbufu

mkubwa kwa wanafunzi wenyewe na wazazi/walezi wao. Vilevile, hali hiyo

inaisababishia Serikali hasara kubwa ya gharama ya maandalizi yote ya mitihani

ya Taifa.

Kutokana na hali hiyo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inaagiza kuwa

mwanafunzi/mwanachuo yeyote asipewe adhabu ya kufukuzwa shule/chuo

miezi mitatu kabla ya mitihani ya Taifa ya kuhitimu ngazi husika ya elimu.

Badala yake adhabu mbadala itolewe kwa wanafunzi ili kuondoa usumbufu kwa

wanafunzi wenyewe na wazazi au walezi wao. Endapo Kamati au Bodi

italazimika kumsimamisha masomo mwanafunzi wakati au ndani ya kipindi cha

mitihani, mwanafunzi huyo asinyimwe kufanya mitihani na badala yake

aruhusiwe kufanya mitihani hiyo katika kituo chake akiwa nje ya utaratibu wa

shule.

Ni jukumu la uongozi wa shule na walimu wote kujua mienendo na tabia za

wanafunzi mapema ili kuepusha tatizo la kuwafukuza shule/chuo muda mfupi

kabla ya mtihani wa kitaifa kufanyika.

Waraka huu unarekebisha mwongozo uliotolewa tarehe 28/03/2011 pamoja na

Waraka wa Elimu wa tarehe 09/12/2011 kuhusu wanafunzi kufukuzwa

shule/chuo inapokaribia mitihani ya taifa kufanyika.

Waraka huu unaanza kutumika mara moja.

M. M. Wassena

KAIMU KAMISHNA WA ELIMU

Nakala:

„h Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI

„h Wakurugenzi, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.