WELL COME ULIMAKAFU SCHOOL WEB SITE.

HOME USAJILI DARASA VII-2012=NECTA MATOKEO YA MTIHANI WAKUMALIZA ELIMU YA MSINGI TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI 2010/2011 MATOKEO YA MITIHANI MUHULA WA PILI-2011 KUMBUKUMBU ZA UONGOZI SAFU YA UONGOZI MASWALI YA JIOGRAFIA VIONGOZI WA SERIKALI YA WANAFUNZI KALENDA YA SHULE RATIBA YA SHULE IDADI YA WANAFUNZI MALI ZA SHULE PICHA ZA SHULE WANAFUNZI WASIO NA SARE MAWASILIANO PICHA ZA SHULE MTIHANI WA ENGISH-STD III MTIHANI FORM TWO NYARAKA ZA ELIMU Photo Blog MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK - KATA YA ILOLANGULU.MARCH-2013

KARIBUNI ULIMAKAFU SHULE YA MSINGI

Ulimakafu shule ya msingi ni moja ya shule zilizopo mkoa wa Tabora.wilaya  ya Tabora vijijini kata ya Ilolangulu Tarafa ya Ilolalangulu Kijiji cha ulimakafu .Katika kijiji hiki kunashule mbili ambazo ni  Kagobole na Ulimakafu.Sulehii inawanafunzi 350 ina walimu 12 wakike wakiume 5

     Shule hii imefanikiwa kufanya vizuri katika shule za wilaya ya Tabora vijijini na imeshika nafasi ya kwanza kwa miaka mitatu mfululizo.Hii ni juhudi za walimu na wanafunzi.

HOTUBA FUPI YA MWALIMU PAUL MEELA KUHUSU MFUMO WA ELIMU.

Ndugu zangu watanzania,

“Mfumo wa elimu ya Tanzania umekuwa ni mjadala wa muda mrefu sasa. Hapo mwanzo, enzi za Mwalimu Nyerere, matarajio na malengo ya mfumo wa elimu ulikuwa kwanza kupinga ujinga. Hivyo basi, lengo lilikuwa kuhakikisha kila Mtanzania anajua Kusoma ,Kuhesabu na Kuandika ili kuweza kujitegemea; “education for self reliance.”Leo hii, tunaweza kuwa na mdahalo wa kujadili mfumo wa elimu katika kipindi cha Mwalimu kama ulifanikiwa au la. Vyovyote vile tukakavyokubaliana katika mwisho wa mdahalo huo, matokeo hayataathiri ukweli — kuwa tulijua kwa dhati malengo na matarjio ya mfumo huo yalikuwa ni nini. Lakini dunia ya enzi zile sio dunia yetu ya leo, hivyo malengo na matarajio hayawezi kuwa sawa, au sio?Dunia imebadilika sana, tangu enzi za Nyerere mpaka hivi leo, mabadiliko haya yakichangiwa vilivyo na utandawazi. Dunia imekuwa kama kijiji kimoja, huku ushindani ukiongezeka kwa kasi kubwa. Malengo na matarajio ya mfumo wa elimu ya Mwalimu Nyerere leo hii yangekuwa hayakidhi mahitaji ya soko la dunia. Kwani, kujua kusoma na kuandika pekee hakuwezi kukufikisha mbali maishani, ingawa ni kitu muhimu.Hivyo, tulianza na mfumo uliohakikisha unatokomeza ujinga. Huo ndio ulikuwa msingi ambao ulijengwa na Serikali ya awamu ya kwanza. Kazi ya awamu zilizofuata zilikuwa ni kujenga kuta, kuweka madirisha, kuwezeka paa, na mambo mengine muhimu yanayohitajika katika ujenzi wa nyumba bora. Nyumba hiyo leo inafananaje? Tujiulize. Kwa maneno mengine, ninaweza kuuliza, malengo na matarajio ya mfumo wa elimu katika awamu zilizofuata umekuwa ni nini? Je, mifumo ya elimu iliyofuata ilikuwa na malengo ya kuchochea ongezeko la shule binafsi, na kuongeza idadi ya wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma nje au ni kuboresha elimu ya Tanzania iwe ya ushindani kama enzi zile?Mimi leo bado sielewi vizuri matarajio na malengo ya mifumo ya elimu iliyofuata baada ya mfumo wa Mwalimu Nyerere imekuwa ni nini hasa. Ninadiriki kusema hilo, kwani malengo na matarajio ya single book system ya Tanzania bado ni tata. Kama matarajio hayo ni kuhakikisha wanafunzi wanafaulu mitihani, basi tumepiga hatua kadhaa nyuma, ndio maana nadhani itakuwa muhimu tukimsikiliza huyu binti katika video hii. Nadhani wasiwasi, maswali na mawazo yake hayapo tofauti sana na yetu, punde suala la mfumo wa elimu ya Tanzania linapowekwa mezani kujadiliwa. Kwa bahati mbaya, Mheshimiwa Rais, Jakaya Mrisho Kikwete hatahudhuria mdahalo wa wagombea urais mwaka huu, hivyo hatuwezi kumuuliza maswali hayo. Lakini ningelipenda sana kujua Nyerere angekuwa na lipi la kusema kuhusu mifumo ya elimu uliyomfuata.”ASANTENI KWA KUNISIKILIZA. 

 

vivutio vya watalii Tanzania

WEBSITES YA WIZARAA YA ELIMU NI WWW.MOE.GO.TZ

Matatizo ya elimu Nchini

Lengo kubwa la elimu ni kumuandaa mtu ili aweze kukabiliana na mazingira yanayomzunguka.Si lengo la elimu mtu kuzunguka na vyeti kutafuta kazi za ofisini tu.Katika fikra za MWALIMU alisema elimu ya Tanzania ni lazima imuandae mtanzania ili aweze kujitegemea mwenyewe ikiwa ni pamoja uwezo wa kuwa na fikra sahihi pamoja maamuzi sahihi(mambo sahihi hutokana na fikra sahihi)
-Asilimia kubwa ya walimu wa Tanzania wamekuwa walimu baada kukosa nafasi kwenye taaluma nyingine.
-Wanafunzi wengi wa shule za msingi wanakaa chini na wengine chini ya miti.
-Walimu wachache waliopo hawana maslahi ya kutosha hivyo wamekata tamaa.
-Asilimia kubwa ya walimu ni wale waliofaulu viwango wa chini sana kwenye elimu ya sekondari.
-Idadi kubwa ya wanafunzi darasani kuliko uwezo wa darasa.
-Shule kukosa nyumba za walimu.
-Kutokuwa na bodi ya walimu.
-Mtihani shule za msingi kuwa na maswali ya kuchagua tu(multiple choice) mpake hesabu.
KWA KUZINGATIA NILIYOYATAJA,LENGO LA ELIMU TANZANIA LINAFIKIWA?

1GOAL Tanzania: Elimu kwa wote

Aliyeko katika picha hapa juu ni  Mwalimu Mkuu Ndugu PAUL MEELA